Wednesday 4th, February 2026
@Ruaha Mbuyuni - KILOLO

Mbio za Kitonga Marathon zimefanyika kwa mara ya kwanza Mkoani Iringa, Wilaya ya Kilolo, Kata ya Ruaha Mbuyuni, ambapo zimefunguliwa rasmi na Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mhe. Benjamin Sitta aliyekua anamuakilisha mgeni rasmi ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mhe. Kheri James.

Mhe. Sitta ameipongeza sana Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo kwa kushirikiana na Chemba ya Biashara ya wilaya hiyo kwa kubuni jambo hilo jema na kubwa kwa mkoa wetu, kwani kwa kufanya hivyo wameweza kuleta wadau wa michezo na uwekezaji pamoja kitu ambacho kinachochea maendeleo kwa kasi.

Aidha kwa upande wake mratibu wa mbio hizo za Kitonga Marathoni Ndugu Mabwende, amemshukuru Mkuu wa Wilaya ya Iringa kwa kutenga mda wake na kuja kushiriki mbio hizo.

Mbio za kitonga Marathoni zimekimbiwa na makundi matatu kwa maana ya Umbali kwa kilometa 5, 10 na 21, ikiwa ni kwa upande wa wanawake na wanaume.

Ndugu Mabwende ameahidi mbele ya mgeni rasmi kuwa mbio hizo zitafanyika kila mwaka mwezi wa kumi ili kuendelea kuitangaza halmashauri ya wilaya ya kilolo kwa kuvutia wawekezaji mabalimbali kwani wilaya ya kilolo ina fursa nyingi za kuwekeza.




Mkurugenzi Mtengaji wa Wilaya
Postal Address: S.L.P 2324 Kilolo
Simu ya mezani: 0262968010
Mobile:
Anuwani ya barua pepe: ded@kilolodc.go.tz
Hati miliki @2017 Halmashuri ya Wilaya ya Kilolo.Haki zote zimeifadhiwa